"Giulia, watoto wengine kwa kawaida huburudika shuleni wakati wa kiangazi. Watoto wa Francesca na Giuseppe wanafurahia sana. Unafahamu vyema kuwa hatafanya chochote kwenye kambi ya majira ya joto! Tunahitaji kutafuta chaguo jingine, kitu ambacho kitamfanya apambane. Hata haonekani kuwa na furaha. Je! Unakumbuka jinsi tulivyokuwa na nguvu wakati tulipokuwa na umri sawa na yake?"
"Bila shaka, naikumbuka!" Mamangu angefoka kwenye mlango wetu kwamba chakula cha jioni kimekuwa tayari. Lakini, mara nyingi, hata singemsikia kwa kuwa nilikuwa na shughuli nyingi kwenye bustani nikijibingirisha kwenye nyasi. Tulikuwa na furaha na huru. Kwa kweli hatuwezi kumpa maisha kama hii mjini. Walakani, hajui jinsi ya kufurahia kambi ya majira ya kiangazi. Hana rafiki, hakuna tunayeweza kumwalika na kumsaidi kuponya tabia hii ambayo anaishi. Haruhusu mtu yeyote kushikamana naye. Wakati mwingine najiuliza jinsi anavyohisi kuhusu sisi. Anakwepa ninapojaribu kumkumbatia..."
"Giulia, vijana hawataki kukumbatiwa na mama zao. Nina uhakika bado anatupenda, lakini hatuwasiliani naye kwa njia mwafaka. Tunahitaji kutafuta njia mpya. Tunahitaji kutafuta njia ya kumuamsha. Labda, angezungumza na Ida? Ana wavulana wawili wadogo. Labda anaweza akatupatia ushauri mzuri. "
"Unaogopa anaweza geuka kuwa kama Libero? Kwamba anaugua ugonjwa unaorithiwa wa kisaikolojia?"
"Hapana, kwa Libero ilikuwa tofauti. Matatizo yake yalitokana na kifo cha babaye. Lakini matukio hayo yanafanana na jinsi Ida anavyofahamu huenda ukafaa. Alifanya miujiza na kijana huyo baada ya kuhamia kijijini. Na alifanya yote hayo pekee yake! na shamba ilisaidia pia."
"Ndio, umjulishe hayo. Naamini dadako. Ana njia yake ya kuangalia mambo, na ninapenda."
"Tutaipata ripoti ya shule lini?" Carlo akamwuliza bibiye.
"Juni 19..."
"Tutakuwa tumechelewa kuamua kitu cha kufanya. Unapaswa kuuliza mwalimu wake wa Italia kuwa na mazungumzo ya moja kwa moja na wewe. Lazima tuamue ni wapi tunapeleka watoto wetu. Maombi ya kujiunga na kambi ya majira ya kiangazi na shule ya majira ya kiangazi yatafungwa kabla ya tarehe 19." alipendekeza Carlo.
"Ndio, umesema ukweli. Tunahitaji kuwa na uhakika wa hali hiyo, ingawa hafanyi vibaya shuleni. Ni vile tu haweki royo yake katika chochote anachokifanya. Unafahamu kwamba wapangaji wapya wameingia orofa ya pili? Waonekana kuwa watu wazuri. Bi Giovanna aliniambia walihamia hapa kutoka Potenza. Hiyo ni mbali! Hakika haitakuwa raisi kwao mwanzoni. Wana mwana aliye na umri sawa na Elio. Nitamwalika aje mchana fulani..."
Giulia kisha akagundua kuwa Carlo, ambaye alikuwa amelala kwenye kochi, tayari alikuwa amezama usingizini.
"Njoo, mpenzi, twende tukalale kitandani." Alimnongoneza kwa upole ili amwamshe.
Sura ya pili
Mnong'ono wa baridi ulikuwa ukimsumbua
Elio alikuwa amesimama kwenye njia pana ya miguu mbele ya shule yake. Watoto wengine wote waliokuwa karibu naye walikuwa wakiongeza kasi, wanaposhuka katika gari za wazazi wao au wakifukuzana wakiwa njiani kwenda nyumbani. Yeye kwa upande mwingine alikuwa akiangalia kila mahali kwa wasiwasi kwa gari ya mama yake kana kwamba ndio njia yake ya kuishi, akitarajia kwamba hajaondoka baada ya kukutana binafsi na mwalimu wake wa Italia.
Baada ya kila mtu kuondoka katika yadi ya shule kwa muda mfupi, Elio aliacha kusubiri na kuanza kutembea kwenda nyumbani. Alichukia kutembea. Na alichukia hata zaidi kutembea chini barabara hiyo isiyovumilika iliyo na mstari wa miti ya ndimu inayounganisha shule na nyumba yao.
Alisubiri dakika chache zaidi na kisha akaamua kuelekea nyumbani pekee yake. Kisha, akamuru mguu wake kusonga mbele. Kwa mtu mwengine yule inaweza kuonekana kama kazi raisi, lakini kwa Elio, ambaye mawasiliano yake na miguu yake ilikuwa haba, ilikuwa mapambano.
Akageuka kushoto kupitia del Corso; akiwa kwa kona alijipata mbele ya barabara iliyonyooka ambayo aliidharau. Kijisitu cha miti ya ndimu ilipandwa kando kando ya barabara hiyo kuu. Kwa mtu mwengine yule ilikuwa tu kijisitu kizuri cha miti ya ndimu iliyochanua ambayo manukato yake yalibebwa na upepo, na kulifanya eneo hilo kunukia viruzi. Alipoanza kwenda chini kufuata mistari ya miti kwa ugumu, alihisi kuwa anafuatwa.
Aligeuka kwa haraka na kufikiria kuwa alikuwa ameona mnyama mweusi amejificha nyuma ya mti.
"Haiwezi kuwa" aliendelea kujirudia mwenyewe. "Je! Nimeona miwani katika pua la mbwa huyo wa ajabu?"
Kwa hofu akaendelea kutembea, huku akiona vivuli nyuma ya miti. Isitoshe, upepo ulikuwa ukivuma kupitia matawi. Mnongono wa upepo ulikuwa unamhangaisha; ilikuwa ikikuna maskio yake na kisha kukwama kwenye akili yake.
Hakuweza kuelewa maana ya sauti hizo. Huku akiwa ameshikwa na hisia hiyo mbaya, aliamuru mwili wake kujaribu na kukimbia. Alikuwa akitokwa na jasho, na akikimbia zaidi, sauti hizo zilizidi kuonekana kama zinamkimbiza na vivuli vikaonekana kuzidi kumkaribia.
Alianza kukimbia kwa kasi na kwa uwezo wake wote. Kisha, alisikia sauti ya kikatili ikimwamuru kuacha kukimbia. Aligeuka mara moja na kwa mara nyingine aliona kitu ya sura nyeusi ikijificha nyuma ya mti uliokaribu. Alikuwa tayari amefika makutano na barabara kuu, ambayo ingeashiria mwisho wa ndoto hiyo.
Hata hivyo, alihisi upepo baridi nyuma ya shingo yake. Aligeuka tena, mara hii bila kukimbia, lakini kitu kilimgonga vikali na kumtupa chini.
Elio alishtuka na kujikunja kama mpira huku kichwa chake kikiwa kwenye mikononi mwake.
Wakati uo huo, alisikia sauti anayoijua ikimwita:
"Elio! Elio! Je! Unafanya nini?"
Ilikuwa dada yake ambaye alikuwa akimkaripia. Alikuwa amekasirika kwa kuwa alikuwa amemkimbilia. Baadaye alitambua kuwa Elio alikuwa katika hali mbaya.
Alitulia na kuuliza:
"Unajisikiaje?"
Elio, baada ya kusikia sauti yake, akainua kichwa chake.
Gaia aligunduwa kuwa alikuwa amechanganyikiwa, anatoa jasho na uso wake ulikwajuka kuliko kawaida. Kwa sekunde, alijaribu kufikiria ni kwanini alikuwa akikimbia. Haikuwa kawaida kwake. Ilionekana kwake kwamba alikuwa akitoroka kitu au mtu. Wakati uo huo, alimsaidia kuinuka.
"Kwanini ulikuwa ukikimbia hivyo?" alimwuliza. "Kuna kitu kilikutisha?"
Gaia hakukumbuka mara ya mwisho Elio alikimbia. Elio hakujibu. Kitu pekee alichokitaka ni kuondoka barabarani haraka iwezekanavyo. Alipiga kona barabarani bila kusema lolote.
Gaia akamfuata akiwa na wasi wasi.
"Elio!" alimwita tena.
"Hakuna kitu!" akajibu Elio kwa ujeuri. "Kwa kweli hakuna kitu!"
Tabia ya Elio ilimfanya Gaia kukasirika tena.
"Hakuna kitu, eeh? Ulinikimbia sawasawa. Na bado, unasema hakuna kitu!"
Elio alimwomba msamahaili kuepuka majadiliano zaidi, only to avoid further discussions, ambayo ingechosha mwili wake hata zaidi.
"Samahani." alisema.
Misamaha hiyo ya juu juu iliishia kumkasirisha Gaia hata zaidi. Hata hivyo, aliendelea kutembea nyuma ya kakaye, huku akiwa na wasiwasi kumhusu.
Kufikia Jumapili asubuhi, Carlo na Giulia hatimaye walikuwa wamefanya uamuzi. Wakati walipokuwa wanatengeneza kiamsha kinywa, walikuwa wakiongea kuhusu wazo hilo wakati wakisubiri watoto kuamka
"Alikuwa mkarimu kutoa wazo kama hilo. Nataraji, hao watato watakuwa na tabia njema." alisema Giulia akiwa na tabasamu kubwa usoni.
Ilikuwa uamuzi ngumu kufanya, lakini Carlo na yeye walikuwa wanahisi shauku ya ajabu kuihusu, kwa vile walikuwa wamekubaliana nayo.
"Gaia atafurahi." alisema Carlo. "Elio, kwa upande mwingine, atasalia kutojali kama kawaida."
"Sina uhakika...Gaia alifanya urafiki na watoto wengine katika kambi ya majira ya joto. Atakasirika. Na kuhusu Elio, atachukia hata hivyo." akasema Giulia.
"Siwezi kusubiri tena. Nitawaamsha." akapendekeza Carlo kwa uthabiti, na kutembea kwenda vyumba vyao akiwaita kwa majina yao.
Hakuniruhusu hata kusafisha uso wao.
"Mama yako na mimi tuliamua kile utakachofanya wakati wa majira ya joto. Shule itafungwa Ijumaa na Jumapili Asubuhi mtapelekwa kwa kituo cha reli!"
Читать дальше